Wizara ya Afya

JUKWAA LA KIDIJITALI LA ELIMU YA AFYA KWA UMMA

Afya Yangu, Mtaji Wangu

Wizara ya Afya

Uhakiki wa Vielelezo

Huu ni ukurasa maalumu unaokuwezesha kupata huduma ya upitiaji, uhakiki na uidhinishaji wa matumizi ya vielelezo mbalimbali vinavyokusudiwa kuielimisha, kuihamasisha au kuishirikisha jamii juu ya masuala mbalimbali ya Afya. Kupitia eneo hili utafahamishwa juu ya ratiba ya uhakiki kwa mwaka mzima, utaratibu wa Kamati ya Uhakiki wa Vielelezo vya Elimu ya Afya kwa Umma, mwongozo na utaratibu wa uandaaji wa Vielelezo kuanzia hatua za awali mpaka usambazaji, pamoja na vigezo vyote vya kuzingatia ikiwemo viambatisho wakati wa kutuma maombi ya uhakiki. Kuhusu uhakiki zingatia kalenda hapa kulia.

Utaratibu na Miongozo ya Uhakiki wa Vielelezo

Ili kuwa na vielelezo vyenye tija katika kutatua changamoto iliyobainishwa kupitia mbinu na mkakati wa mabadiriko ya tabia jamii na uelimishaji, tafadhali zingatia taratibu zilizo ainishwa katika muongozo “SOP” pamoja na hadidu za rejea zilizoambatishwa hapa chini. Aidha, mchoro katika mkono wa kulia unakupa dibaji ya utaratibu mzima wa uhakiki.

Maombi ya Uhakiki na Vibali

Tumia kitufe "Maombi ya Uhakiki" kulia ili kuwasilisha maombi ya uhakiki wa Vielelezo vilivyoandaliwa. Aidha, kabla ya zoezi la uwasilishaji wa maombi ya Uhakiki, unahimizwa kujiridhisha juu ya vigezo na uwepo wa viambata vyote vilivyobainishwa katika ”checklist” iliyopo hapa chini..

Checklist for Submission of IEC/SBCC materials checklist

CATEGORY A: ADMINISTRATIVE
  1. Official application letter with name of contact person (E-mail & mobile phone)
  2. Attached filled submission check list
  3. Attached filled application form found in the MoHCDGEC/IHPDP website
  4. Attached evidence of paid application fee  (ie. paying slip)
Edit Page

WASILIANA NASI

Jamhuri ya muungano wa Tanzania

Wizara ya Afya

Mji wa Serikali - Mtumba,

S.L.P. 743,

40478 DODOMA.

+255-22-2342000/5

ps@afya.go.tz

Call Center: 199 | *199#